Saturday, March 24, 2018

Unakuwaje Mjasiriamali?

Miaka ya hivi karibuni pamekua na wimbi la watu wanaojiita wajasiliamali ama kwa sababu wanafanya biashara ndigondogo ama kwa sababu hawajaajiriwa.
Hii ni kwa sababu ya dhana iliyojengeka kuwa wajasiriamali ni watu wenye biashara ndogo ndogo na duni.

Bila ya kujali udogo au ukubwa wa shughuli ya kipato ujariamali ni ujasiri katika kushughulikia mali.

Tofauti na wafanyabiashara , wajasiriamali wana mtizamo tofauti juu ya uendeshaji wa shughuli za kipato. Uimara na mtizamo wao juu ya mambo unawatoa wao katika kundi la wafanyabiashara na kuwa wajasiriamali au kuwa wafanyabiashara wajasiriamali

Sifa kubwa ya mjasiriamali ni UJASIRI,katika kusimamia lengo lake, pia ubunifu kwa kila jambo lijalo akilini mwake halifanyi katika namna ya kawaida kwa maana hulipa thamani,uthubutu ni jambo jingine ambalo ni sifa ya mjasiriamali. Hana ngoja ngoja hana mipango iliyokithiri na isiyokuwa na mwisho.Anapopata wazo hulifanyia kazi mara moja.

Jambo jingine ni uvumilivu. Siku zote mjasiriamali hakati tamaa , kila analolianzisha basi atalisimamia licha ya magumu yote atakayopitia atahakikisha linakua.Licha ya kwamba atadondoka mara kadhaa.

Hizo na nyingine nyingi ni sifa zinazimtrngezeneza mjasiriamali.

HATUA ZA KUWA MJASIRIAMALI

1.JITANBUE WEWE NA UWEZO WAKO

Ndiyo,hatua ya kwanza kufikia ujasiriamali ni kujitambua wewe na uwezo wako. Jua una uwezo gani,yajue maarifa yako,inue nguvu yako.Fursa zote ambazo unaweza kuzifikia zinaanzia ndani yako.Wewe ni zaidi ya mashine,akili na mwili wako vina nguvu zaidi ya unavyodhani.Unapojenga wazo lijenge kulingana na vipawa ulivyonavyo na kisha jiulize "je napenda kufanya hivi?" Hapa utashangaa maajabu ya ubongo wako.

2.TAMBUA/TENGENEZA FURSA
Hawi mjasiriamali mpaka awe na uwezo wa kutambua na kutengeneza fursa. Mjasiriamali ana jicho la tatu juu ya kila kitu kwani anaona mbali zaidi.Watu wanaposhindwa yeye huona njia,changamoto za watu yeye kwake huwa ni fursa.
Ila pia huwa na uwezo wa kulitengeneza jambo na kuwa fursa.Pengine watu hawakuwahi kulifikiri jambo ila mjasiriamali hulileta na kuligeuza kama jambo watu wanalolihitaji.
Mfano jiulize swali "je watu waliishi vipi kabla ya ujio wa televisheni?" Ajabu terevisheni imekuja kuwa kitu muhimu sana kwa binadamu.Huu ni mtizamo wa kijasiriamali.

3.BUNI MBINU ZA KUFIKIA MALENGO
Umetengeneza ama kung'amua fursa. Vipi endapo utaamua sasa kulifanyia kazi kwa kutafuta namna ya kufikia malengo.Kaa china na chora ramani ya namba ya kufikia lengo.Ramani hii si ya kukumalizia muda weka muda unaofaa kulifanyia kazi,isiwe mwaka mzima unapanga , la panga kwa wakati ,buni mbini A,B na hata C.Pigania kufikia lengo.


4 TENGENEZA /TAFUTA MTAJI
Changamoto namba moja ya wafanya biashara ni mtaji wa pesa, ila changamoto namba moja ya mjasiriamali ni wazo na fursa. Pesa ni mtaji ila mtaji namba moja ni akili.Fikiri binadamu wa kale waliishi karne nyingi sana kabla ya kuanza matunizi ya fedha, je waliishije.Mahitaji ya fedha huja baada ya matumizi sahihi ya akili na uwezo wake.
Ndiyo pesa inahitajika ila si jambo kubwa kama akili.Mtuzame dalali wa nyumba na viwanja anaendesha maisha yake kwa kuwa na taarufa tu za muuzaji na mnunuzi kisha kuwakutanisha naye kupata mkate wake.Mtaji wake mkubwa ni taarifa.
Pesa iwapo kidogo weka mikakati ya kuikuza ili kufikia hitaji la ujasiriamali.Hapo utakua umeinesha UJASIRI na kamw hutashindwa.

5. ANZA MARA MOJA
Unakumbuka msemo wa ngoja ngoja huumiza matumbo?Ndio kukawia kufanya jambo kwa kukawia kupanga ni kiashiria kikubwa cha kushindwa. Umalizapo mikakati yako anza shughuli yako mara moja.Usiiruhusu akili yako kutota kwenye hatua ya kupanga, THUBUTU mara moja licha ya changamoto zinatokea ubongoni ushinde uwoga na anza kufanyia kazi wazo lako mara moja.

6. KUZA SHUGHULI YAKO
Mjasiriamali habweteki ,kila jua lichomozapo huwa na wazo jipya la kukuza na kuimarisha shughuli zake.Ubunifu wa bidhaa mpya na mbinu mpya za masoko ndiyo mambo muhimu mjasiriamali hufanya kila siku.Mjasiriamali ni mtafiti na mdadisi na anaependa kujifunza.Hivyo bidhaa au huduma zake hiwa bora kila wakati kwa kulenga mahitaji ya mlaji.

7. JIONE MBALI
Wewe pamija na shughuli zako mjione mmefika mbali lenga picha kubwa wa shuguli yako na hakikisha unafika huko kwa kila hali.Changamoto zipo na zitakuwepo tu ila zisiwe kizingiti cha wewe kupaa.Hakikisha una ndoto kubwa.

8.KUWA NA MTIZAMO CHANYA.
Mara nyingine mambo huwa hayawi vile tumeyatizamia kuwa,mambo yanapokwenda tofauti ona kama ni fursa ya kujifunza,furahia changamoto kwani ni darasa zuri. Msemo wa kiswahili uliobeba ujumbe ,Yaani "lisilokuua basi litakujenga" kubali kunengwa na changamoto na si kukubomo.

Kwa kuweza kuyahimili haya ,kwa liasi kikubwa utakua umeweza kujijenga kama mjasiriamali.Simamia wazo lako hata kama ni dogo kiasi gani hilo ndilo lako.Usiruhusu woga na mashaka kulegesha maono yako.

"Wewe ni mshindi"

Tukutane katika makala nyingine kujadili changamoto na namna ya kupambana na changamoto za ujasiriamali.

Imeandaliwa na :
Abdallah Wihenge J.E
Teainer / Facilitator
+255 716 050

Wednesday, March 21, 2018

Youth Empowerment

World population grows up to 1.09% in every year ,This means number of population increase every year and world resource seemly to remain scarcity. This imply that human being has to work even harder to make sure that s/he obtain at least quadrant of his demand and needs.
Scarcity of resource is not as same as scarcity of opportunities. Since world population increase and people have to suffocate to obtain their demand,it reflect that needs and demand increase each day and night thus someone demand is someone opportunity. It is not easy each one to satisfy his demand that why it referred someone demand is someone opportunity.
Youth constitute approximately 18% of world population. But the question comes is that population bring impact to the world development? In some extent its yes but not as it should be, youths were faced with various challenges that undermine their impact to the world development. 20% of all youth in the developing world are not in education, training, or employment. Here another question rose is education and trainings are the only solution to the youth development? It is not , because there are number of youths received formal education but they stay unemployed and not productive. Here each world youth support organization and youths themselves should brainstorm on the causes of the situation in order to overcome it.
Partially, youths were faced with various challenges on making them productive apart from the fact that some of them receive formal and informal education and trainings. Basing on areas, in sub Saharan Africa , youth were not prepared to be productive base on the education systems,society,policies and information. Youths think of only single channel to create impact to the development and that is that what they taught in schools and colleges. They were not equipped with knowledge that will allow them to adopt global changes in economic and social matters. It is worse for those with no formal education and training they are brain stacked with no idea what to do.
Looking to other side, training on self reliance and entrepreneurship is provided to those youths , but its only to some of the targeted number. Information is only available for those with platform to obtain those information but to those in rural areas and those with no platform it is great challenge. Unfortunately even for those received education and training fall to another trap , they lack financial support ,follow up and mentor ship, therefore no impact created.
To solve youths' development issues require to dig in to the roots and time investments and research, but for youth they have to start personal improvement efforts to make sure that they become productive to their societies and world at large. They should organize themselves and create platform were everyone will share his/her potential to reach personal development goal.Some have information but they have no idea on how and where to use it,some with knowledge and skills of doing things but they lack information on where they will apply their skills. By joining it will create least impact to their lives.
To get support from development organization need to be organized. Youths should learn how to organize themselves even for small projects there they will start to have at least initial to big project.
Youths issues are very wide and complex, they should be discussed in a very often bases.This small article aim to introduce some of the issues faced by youths ans some partial solution.In the coming articles more problems and solutions will be arose basing on comments and readers recommendation.

Prepared by: Wihenge,Abdallah J.E
Corporate trainer and facilitator
Email:abbshey09@gmail.com
+255 716 050 555

Monday, March 19, 2018

Nguvu ya Asante

Unaijua nguvu ya asante?
Katika kipindi cha ukuaji tangu tuwapo wadogo, kati ya maneno ya mwanzo kabisa kujifunza ni kusema asante. Je hukuwahi kujiuliza kwa nini wazazi au walezi hukazia hapo na kutaka mtoto ajue kusema asante? Pengine hata wao hawajui,kutakua na fumbo kubwa sana ndani yake.
Nini maana ya asante ?
Pengine ni neno ambalo ni la kawaida sana na ambalo tunalitumia mara kwa mara pale ambapo tunakua na lengo la kuwasilisha hisia njema juu ya mambo tunayofanyiwa ama kupewapo. Upana wa neon asante msingi wake ni kuelezea kujali,kutambua thamani,heshima,shukrani, na mengi ya kufanana na hayo.
Kila binadamu hata akiwa ni mkatili au mkaidi wa kiasi gani,huona fahari kusikia maneno mazuri ikiwa ni pamoja na asante hata kwa dogo alilolifanya akiamini kuwa ni jema ,hapa ataona thamani na kuheshimiwa kwake. Katika nyakati za ugumu neno asante hudumisha uhusiano na mwendelezo wa mambo mema baina ya watu ama makundi ya watu.
Katika utamaduni wa watu wa magharibi tangu miaka ya 1800 wamekua na siku maalumu kwa ajili ya kusheherekea asante wakiita kama “thanksgiving”. Kwa kuuona umuhimu wa asante imekua ni utamaduni wa kudumu na umerithishwa vizazi na vizazi. Sherehe hizi zimekua zikisheherekewa kwa watu kukaa pamoja na familia au jamaa na kuzungumza pamoja na kupeana shukrani kwa mambo mema yaliyotokea katika kipindi cha mwaka mzima, kula chakula kwa pamoja , kucheza pamoja na pia kufanya shughuli mbalimbali kwa pamoja.
Kwa kufanya hivi imekua ikileta athari njema kwa familia na koo zao kwan hudumisha umoja na ushirikiano wa kifamilia na kusuluhisha migogoro endapo ilitokea.
Katika utamaduni wa kiafrika imekua kawaida kujifunza na kusema asante japo utamaduni huu unazidi kuathiriwa siku hadi siku kutokana na sababu mbalimbali ambazo tunaweza kuzirejea kama si sababu za msingi. Moja ya mambo yanayodidimiza utamaduni huu ni aina ya malezi ambayo yamekua yakitolewa na wazazi wa kizazi hiki kwa kuamua au kusahau kutilia mkazo juu ya kusema asante. Pengine kwa sababu tu tumekua tukijifunza na tukifundisha kusema asante kwa sababu ni utamaduni tuliorithishwa na wazazi au ni jambo tu la kawaida ambalo huwa tunalifanya na kuona ni la kawaida tu kama maneno mengine.
Kuna haja ya kwenda mbali zaidi na kutizama je kuna umuhimu wa kusema asante na kwa nini tunasema asante.
Athari za neno asante.
Neno asante lina uwezo la kuhamasisha na kutia nguvu ndani ya watu. Umewahi kufikiri juu ya mtoto anaetumwa na mama yake akalete chombo ndani ama kwennda dukani na sokoni kununua bidhaa fulani kisha mama akamwambia asante? Pengine angeweza kumtuma mara nyingi zaidi bila ya mtoto kuona kama amesumbuliwa, angeweza kwenda tena na tena kwa kuona tu mama anatambua mchango wake au utendaji wake.
Hivyo hivyo pindi anapopokea mtu msaada na kasha akasema asante , basi atakaetoa msaada anaona wazi kabisa kuwa amefanya kitu cha thamani na ataona umuhimu wa kufanya tena na tena.
Utafiti uliofanyawa na chuo cha Georgia nchini Marekani juu ya masuala ya ndoa kauli ilitolewa na watafiti ilisema “tumegundua kwamba kutambua thamani ya mwenzi wako kwa kumshukuru kwa kila jambo,inaongeza nafasi ya kudumu kwa muda mrefu na kuona kwa kiasi gani pande mbili katika ndoa zimeivaa ndoa vilivyo”. Hii inamaana ataweza mtu kuvumilia zaidi na zaidi ndani ya ndoa yake kwani thamani ya mema anayoyafanya yanaonekana na kutambuliwa.
Kushindwa kusema asante
Kushindwa kusema asante kunapelekewa na mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuona ya kwamba tumeridhika,ubinafsi,ukosefu wa malezi bora, kujiona ni bora zaidi ya wengine na kadhalika.
Kushindwa kusema asante humfanya mtu kuonekana ana majivuno na kiburi. Mahusiano baina ya watu huathirika kwa kushndwa kusema asante. Hatafanya mtu jambo kubwa au hata dogo akaona kafanya pasito na watu au mtu kutambua amefanya kitu.
Katika kuboresha maisha yetu na vizazi vyetu busara zaidi kjifunza kusema asante hata kama si jambo kubwa au kitu kikubwa ambacho tunapewa.Mahusiano baina yetu utu na uungwana ni matunda yatakayotokana na kujifunza na kusema asante kwa dhati.
Asante ya dhati
Kuna namna mbali mbali za kufanya asante kuwa na sura ya dhati na iweze kuleta uchanya pale ambapo inatolewa . kwa mapendekezo hizi ni namna bora za kusema asante ya dhati.
Iseme kwa lengo mahususi.
Kusema asante tu bila kusema asante inahusu nini ni jambo unalolishukuru.Mfano “mama, asante sana kwa kuninunlia zawadi ya kitambaa nimeifurahia sana” hii itamgusa moja kwa moja alieshukuriwa na kuona uzito na thamani ya kile ambacho amekifanya na ataona munganiko na furaha ndani yako. Isisemwe asante inayoning’inia na kuacha maswali ya hasa nini mtu anashukuru? Kwa kiasi gani asante umeguswa na wema uliotendewa.
Ushiriki wa mwili na viungo
Kusema asante hali ya kuwa umenuna au ukiwa na kisirani haiwezi kuwa asante ya dhati. Ni vyema unaposema asante umaanishe na mwili mzima onyesha muunganiko wa asante na mwili wako na uso uoneshe ya kuwa unamaanisha. Vitendo husema zaidi ya maneno, hivyo itende asante yako na ionekane.
Chagua mahala na muda sahihi
Wakati unataka kusema asante sharti kuchagua mazingira sahihi ya kusema asante, Si mahala popote unaweza kusema asante. Iseme wakati inatakiwa kusemwa kisipite kipindi kirefu kabla ya kusema asante kwa wema uliotendewa leo.
Ili kupata zaidi tukumbuke kusema asante na tuwakumbushe wengine kusema asante, Makuzi kwa watoto wetu yaambatane na kujifunza kusema asante pia tuseme asante ya dhati na si asante ya juu juu kwa maana tumaanishe tusemapo asante.
Kumbuka “Mara nyingi huwa tunakumbuka sana pale mtu anaposahau kusema asante ,hasa ambapo umetumia muda na nguvu kumsaidia , hapo ulipo umekumbuka tukio kama hilo”
Imeandaliwa na Abdallah Wihenge

KOMAZA TABIA NJEMA


Habari,
Katika kipindi cha miaka mitatu ya kujifunza namna ya kubadilisha mfumo wa maisha yangu nimejifunza mambo mambo haya yaliyonijenga kitabia.Leo tutayaona hapa kwa ufupi ili pengine kila mmoja wa wakati wake anaweza yatumia kama mbinu ya kujenga tabia yake.
1. Jifunze kusikiliza zaidi ya kuongea.
Mara nyingi unapoongea basi unatoa kile ambacho unakielewa na kukifahamu ila hakuna unachoingiza kichwani mwako zaidi ya unanchokifahamu.Kwa kusikiliza utaongeza kitu na kwa kusikiliza sana basi itakuongezea maarifa na ujuzi.Na sharti kubwa la kusikiliza ni kusikiliza ili kuelewa na si kusikiliza ili kujibu.Kwa kusikiliza bila kufikiri kujibu utaipa akili yako uwanja wa kujifunza na kupokea jambo.
2. Kuwa na mtizamo chanya
Haitatokea siku kwa asilimia mia moja kila amabalo utalipanga litatokea namna ulivyolipanga.kuna wakkati mambo huwa tofauti na vile tulivyotegemea au kupanga.Huu ni wakati wa kuona kuna nafasi ya kujipanga upya na kuona si bahati mbaya na ilipaswa kuwa hivyo.Kushindikana kwa jambo ni hatua ya kuwezekana na ni hatua ya kujifunza,jambo kwenda vibaya ni matokeo ya muda mfupi si wakati wa kujisikia vibaya na kuchukia wengine au wewe mwenyewe.Kila jambo linapotokea hata kama halilidhishi basi litizame katika upande wake mzuri.Kila baya linalotokea lina uzuri ndani yake na huo ndio wa kuutizama kwanza kabla ya ule mbaya hata kama upande mbaya ni mkubwa. kumbuka "lisilokuua basi litakujenga"
3. Jifunze Kusamehe
Kuwa na vinyongo,hasira,visasi na mafundo ni ugonjwa wa vidonda ambao dawa yake ni kuviacha hata kama ni mtu mwingine ndiye aliyekusababishia hayo.Kusamehe kunatibu ugonjwa huu na kuupa moyo amani ya kusonga mbele.Kutokusamehe ni kuubebesha moyo mzigo usio wa lazima.Uliyekosewa ni wewe na mwenye maamuzi ya kusamehe na kujitibu ili usonge mbele ni wewe.Usibebe magonjwa yasio na ulazima samehe upone.
4. Amini unachokifanya na weka mipaka juu ya kuwaamini wengine.
Mtu wa kwanza kumuamini ni wewe,Ndio ni wewe kama wewe utashindwa kujiamini hakuna wa kukuamini.Kila ambalo unaamini unaweza ni kweli unaweza,changamotoipo ila amini unaweza,Asikuangushe mtu amini amini unaweza.Ila usiamini misingi au misimamo ya mtu kama ndo jibu la mwisho utakachosika au kusoma au kupatia taarifa kisiwe kamando jibu la mwisho kabisa.Rudi nyuma chambua na uchanganye na mambo yako kabla ya kukubali au kuunga mkono.
5. Kubali kukosolewa
Kwa namna ya kipekee ambayo binadamu ameumbwa , haikuwahi kuwa kweli kwamba hakuwahi kukosea.Kukosea ni jambo moja na kukubali kwamba umekosea ni jambo jingine.Kuyakubali yote ni hatua kubwa katika kujiimarisha kitabia.Kukosea si vibaya kwani kujifunza huanzia hapo na hauwezi kujifunza kwa usahihi bila kukosolewa.Unapokosolewa jione una bahati na ni nafasi ya kukomaa zaidi.ukiona kila unachokifanya unaambiwa upo sahihi rudi nyuma na ujiulize kwa nini naambiwa haya na moja kati ya haya ndio majibu ya hali hiyo.Ama unabezwa,ama unaogopwa ama kuna maslahi anayoyapata mtu kwa kukubalinana na kila wazo lako.
6. Fanya maamuzi
Ndiyo, Fanya maamuzi bila kuhofia sana juu ya athari za maamuzi hayo ilhali tu unaamini kileunachokifanya kipo sahihi.Kama ni biashara anza biashara, kama ni mradi fanya mradi usiwe ni mtu wa kurejea nyuma mara kwa mara na kuanza kutengeneza picha ya namna itakavyokua baada ya kutenda tena mbaya zaidi picha hasi juu ya nini kitakua.Watu ambao hufanikiwa zaidi ni wale wanaoamua kwa wakati bila kujiogopesha na kutoa muda kwa mambo yasiyokuwa ya msingi.Hakikisha unafanya kitu sahihi katika wakati sahihi na siku zote utayaona matunda ya hilo.
7. Saidia wengine
Njia kubwa ya kujiimarisha na kujikomaza katika tabia njema ni kusaidia wengine,hapa utajenga uwezo wa ndani.Hili ni kama zoezi la kujijenga kama una maarifa juu ya jambo kwa kuwasaidia wengine basi utayakumaza maarifa yako ila kama ni jambo unaaidia wengine basi utajijenga ikiwa ni pamoja na kutengeneza mahusiano mazuri na furaha kwa wengine.
Katika makala ijayo tutaona nini maana ya mafaniko kwa sehemu yake kwani ndiyo kitu ambacho kila mmoja wetu anapoamka anahangaikia kukipata kwa namna yoyote,japo wengi wetu hatufahamu tafsiri ya kweli ya mafanikio.
 
Abdallah Wihenge J.E
Trainer/Facilitator

Dondoo: Namna ya kuajirika.


Vijana wengi tumekua tukilalamika ya kuwa hakuna ajira ,jambo ambalo kwa namna moja ama nyingine ni kweli. Si wote katika vijana hawapati ajira kwa sababu tu hakuna ajira isipokuwa wengine hawapati ajira hata ajira zinapokuwepo.
Ila kwa ajili tu dhana ya kwamba ajira hamna imejenga kambi katika akilini basi hapatafutwi sababu nyingine ambazo zipo wazi kwamba pia VIJANA HAWAAJIRIKI.
Ukipata fursa ya makampuni na mashirika yakituma matangazo na kuyatangaza tena na tena kutafuta watu wa kujaza nafasi fulani hujawahi jiuliza kwa nini?
"Re advertised" tumeona tena na tena,je wanapenda tu kufanya hivyo?
Ukweli ni kwamba wanatangaza nafasi,watu wanaomba na bahati mbaya hawampati anaefaa. Hapa ni kwamba vijana hawana sifa, japo wamesoma wana vidato,vyeti,shahada,astashahada n.k na wengine uzoefu wanao.
Kwa nini haujaririki. Ukijiuliza hili swali na kujitathmini utakua umepiga hatua kubwa sana kuelekea kwenye kuajiriwa.
Hapa kuna dondoo chache la kukufanya uajirike kwa wenye ndoto za kuajiriwa.
1. Jifunze jambo jipya kila upatapo nafasi.Ama kwa kusoma vitabu vinavyojenga,majarida,magazeti,vile vile jifunze kwa waliokizidi na uliowazidi.
2. Tengeneza mtandao wa kitaaluma. Hakikisha watu wanaokuzunguka ni wataaluma wa mambo fulani fulani na yatakusaidia kujifunza kupiga hatua ikiwa ni pamoja na ushauri.
3. Tumia vyema mitandao ya kijamii.Hapa vijana wengi tumepotea.Usitume mtandaoni juu ya maisha yako ya ndani au mavazi yako au uzuri wako.Wapo wazuri wengi na hawajatuma picha mtandaoni wamebanwa na kutafuta maisha. Kwa bahati mbaya muajiri akiona unayoyafanya mtandaoni ataona kwa kiasi gani haupo "smart"
4. Jitolee kwenye miradi,makampuni na mashirika mbalimbali.Yatakujengea uwezo wa kujiamini na uwelewa wa mambo kwa nadharia na vitendo.
5. Usiogope kujaribu kwa kila jambo ambalo halivunji sheria na lina mlengo wa kukujenga na kujenga wengine.
6. Uombapo nafasi katika kampuni au shirika hakikisha wasifu (CV) yako imeandikwa kwa kukidhi viwango vya uandishi wake.
7.Epuka kuomba kazi ambayo haukidhi vigezo,unajitengenezea mazingira ya kukosa ajira hata kwa kazi nyingine katika shirika/kampuni husika ambayo ungekidhi hiyo ni "unprofessional"
8. Jiandae kabla ya usahili usikalili kabla ya usahili. Na usi "panic".
9. Usiamini ya kwamba elimu yako ndicho kigezo kikubwa cha wewe kupata ajira. Ajira ni nini ulochonacho kichwani na wala si matokeo ya darasani.
10. Usikate tamaa. Fanya zaidi na zaidi buni njia mpya ya kupata ajira kila unaposhindwa katika mbinu nyingine.
Kumbuka : Suluhisho kubwa la kukosa ajira ni kuajiri wengine kwa maana tengeneza ajira. Jifunze kutengeneza ajira.
Katika makala nyingine tutajifunza namna ya kutengeneza ajira.
Asante.
Imeandikwa na :
Abdallah Wihenge J.E
Trainer / facilitator Brac Tanzania
+255 716 050 555