Wednesday, September 5, 2018

Njia katika kufikia ndoto zako

Kwa wenye imani wanaamini kwamba hakuna jambo linaweza kukutokea katika maisha ila ni mipango ya Mungu. Ni kweli kabisa ama mambo yakaenda vibaya ama vizuri Mungu ana nguvu juu ya mambo hayo.Hakuna kitu katika maisha ya binadamu kinatokea kwa bahati mbaya ila ni nguvu binafsi iliyosimamiwa na uwezo wa Mungu.
Haimaanishi kwamba kwa kuwa kila kitu kipo mikononi mwa Mungu basi inatosha kabisa kukaa chini na kungoja ama miujiza au neema ya Mungu ikushukie ,inakupasa uweke juhudi katika kukamilisha majukumu na shughuli zako
Mantiki hasa ya kuandika makala hii fupi ni kusisitiza kwamba hupaswi kukata tamaa kwa kuamini kwamba Mungu hakupanga. Ni kweli Mungu ni mpangaji wa kila jambo ila kumbuka ya kwamba hata alilolipanga hawezi kulifanya likawa muujiza ni lazima ulitolee jasho na kulitilia juhudi.Tizama matajiri wengi mapito na changamoto walizopitia mpaka kuwa matajiri , haikuwa rahisi kwao kufikia malengo ambayo naamini kwamba walipangiwa na Mungu ila waliyapata baada ya kupitia changamoto hizo na kuanguka mara kadhaa. Tizama watu wasomi na wenye maarifa makubwa haikuwa rahisi kwao kuyapata maarifa hayo isipokua kwa kuwekeza muda na nguvu katika kujifunza na kufundishwa.
Siamini ya kwamba Mungu aliumba watu kuwa maskini au matajiri ila nguvu na jitihada ndizo zitakazo amua uwe wapi.Hakupanga watu kuwa wajinga au welevu ila ni kwa kiasi gani walitumia nguvu na akili zao katika kujijenga.
Inawezekana haufanikiwi katika jambo fulani, ndiyo haufanikiwi ,je umewahi kupata fursa ya kukaa chini na kujiuliza kwa nini haufanikiwi?Je ulipojua kwamba haufanikiwi ulifanya jitihada gani kupata suluhisho?
Inawezekana kabisa ukawa hauna namna ya kutatua matatizo ila kwa kujua chanzo cha tatizo na njia za kutatua tatizo japo haujalitatua ni hatua kubwa sana katika kufikia malengo ya maisha yako.
Kufanikiwa kwenye jambo lolote kunahitaji maombi,jitihada na kujitoa.Ukijumuisha haya na mengine mengi yanayohitajika basi kile tunachokiita kuwa ni mpango wa Mungu kitatimia.
Katika kufanya mambo yako na ili yafanikiwe kwanza ondoa shaka kwa kuamini katika kile unachokifanya,tumia maarifa yanayohitajika na kama hauna basi jifunze,wekeza muda wako endapo tu umekwisha amua na kutambua usahihi wa ukifanyacho,amini katika matokeo pia kwa maana matokeo ndio yakayonesha umeweza au la, na la mwisho usiogopeshwe kwani kila mtu ana anachokiamini na anachokiweza.
Kumbuka Kuwa na mtizamo chaja kwenye mengi ya mambo yako,kila mtu kwa wakati wake aliumbwa kuja kufanya kitu cha kipekee hapa duniani hivyo fuata yako kwa wakati wako kwani ndicho ulichotumwa kuja kukifanya duniani.

Kwa maoni ama ushauri usisite kutoa maoni kupita

barua pepe :abbshey09@gmail.com