Imeandikwa
na Abdallah Wihenge | Dodoma
Siku
kadhaa zilizopita nilipata fursa ya kumsikia moja ya wazungumzaji mashuhuri
sana Chris Mauki katika ukanda wetu wa Afrika mashariki katika kipindi cha
redio na alikua akielezea jambo juu ya kuwa na maono,mipango na kujituma ama kujiongeza kwa kwenda hatua ya ziada
katika mambo ya kimafanikio. Katika msingi wa maelezo ya mzungumzaji alielezea
juu ya umuhimu wa kujitafakari na kujenga picha kubwa ya maisha yajayo na hii
hainzii ukubwani ni jambo ambalo linakita mizizi tangu katika kipindi cha
makuzi.
Kwa
mantiki hii ni wazi kabisa wengi katika jamii nyingi za watu weusi wamekwishakawia
katika kutekeleza makusudi ya maisha yao na wengi wanajikuta wanaongozwa na
mfumo na kasi ya maisha na si wao ambao wanaoendesha maisha yao. Matukio na
misukumo tu ya maisha ndo humfikisha mtu mahala Fulani ama pakubwa au padogo
inategemea tu na ‘zali’ lake.
Ujasiriamali ni kichaka
kipya cha kukimbilia?
Kulingana
na hali ya maisha imekuwa utamaduni au mazoea sasa hivi watu kujificha kwenye
kichaka cha ujasiriamali pale ambapo kila kitu kimekwenda mrama. Mfano kijana
amesoma na akakosa ajira basi ataingia kwenye kichaka cha ujasiramali,mtu
akapigwa na maisha vilivyo basi nae kichaka hiki humuhusu. Kwa maneno yasiyo
rasmi tunaweza kuita ujasiriamali ni neno jingine la ukosefu wa ajira. Na
mkwamo huu ni kiashiria tosha kwamba wengi ya watu katika jamii zetu hawafahamu kusudio la maisha yao. Ni maelekezo
na mfumo tuliopewa ama na wazazi,walezi au jamii juu maisha. Wengi ya wanajamii
hawaishi maisha yao ndani ya kusudio isipokua mfumo ulioweka na jamii na
familia.
Katika
kukielezea kichaka hiki cha ujasiriamali na biashara, moja ya waandishi
mashughuli wa masuala ya biashara na ushirika aliwahi kuandika “Kwa
miaka ishirini iliyopita, anaelezea jinsi kila siku, zaidi ya mawazo elfu mbili
hujaribu kuanzishwa kama biashara, lakini kwa mwaka mmoja, ni asilimia tano tu
ya kampuni hizi zilizosajiliwa zinaishi na kukua”

Katika
mazingira niliyoyataja hapo awali ni wazi kwamba wengi watu wengi hivi sasa
hawana mpango,mkakati wala kusudio la maisha yao isipokuwa ni maisha yenyewe
ndio yataamua wao wawe nini.
Kusudi la kuandika Makala hii fupi ni
katika kuona ni kwa namna gani kuweka lengo la maisha kunaweza kukupa picha na
njia ya maisha yenye mafanikio. Na ikumbukwe kwamba mafanikio si pesa tu, ni
mkusanyiko wa mambo lukuki ambayo hayo tutaayandika katika Makala
zitakazofuata.
Katika
umri Fulani wa maisha akili ya mwanadamu huanza kufikiria kwa namna gani ama ni
shughuli gani mtu anaweza ifanya ili aweze kufikia malengo Fulani ya maisha au
kujipatia kipato na kuendesha maisha.
Gundua kusudio lako la maisha sasa!
Kusudio
la maisha huanzia hapa katika kuchagua nini cha kufanya na namna gani ya
kufanya ndipo watu wengi hupanda kipando kisicho sahihi katika kufikia malengo
ya maisha yao na kwa namna wanaweza kufanikiwa.
Kipando au njia sahihi ndiyo
itakayomfikisha mtu pahala sahihi kimaisha, ila kushindwa kujua upo duniani kwa
lengo gani au wewe ni nani basi kwako maana ya maisha itabaki kuwa ni pumzi.
Baadhi ya watu ni matajiri wakubwa na wamiliki wa makampuni makubwa ndani yao
na ndio kusudio la kuumbwa kwao ,ila kwa kushindwa tu kutambua hilo wao
wamebaki kuwa masikini na mafukara wakubwa. Lewis Carol, mwandishi mashuguli wa
miaka ya 1800 aliwahi kusema “Ikiwa haujui unaenda wapi, barabara yoyote
itakufikia “. Kwa mtazamo huu
mtu asitegemee kupiga hatua ikiwa hajui kusudio la maisha yake ni nini.
Katika
mchakato mzima wa kufikia kusudio sahihi linakuwepo ndani ya mtu na uwezekano
wa kutimilika kun maswali yanamjuzu mtu kujiuliza na kasha kuanzia hapo ule
mchakato mzima wa kuyafikia malengo ya maisha na mafanikio huanzia hapo.
·
Kitu kipi unakihitaji sana?
·
Jambo gani linakufikirisha sana?
·
Kwa namna gani unatumia pesa zako?
·
Namna gani unatumia muda wako?
·
Ni akina nani unafurahi kushirikiana
nao?
·
Kipi kinakufanya ucheke?
Mambo
haya yapatayo saba ni kichocheo kizuri sana katika kuyafika makusudi ya maisha
na mafanikio. Ni moja ya funguo kubwa
katika kufungua makufuli na vifungo na ubongo wa kila mwenye nia thabiti ya
kutaka kupiga hatua.Hakuna atakayekua na na mafanikio ya kweli isipokua yule
anaefanya kitu ambacho yeye ni shauku (passion) yake kuyafanya.
Ngoja
nikwambie, ifahamike kwamba mambo mengi tunayoyafanya si lengo la kuwepo kwetu
isipokua kutokutambua tu ndio kunatupeleka katika lengo lisilo sahihi la maisha na ndio tunalalama na kukosa
mwelekeo yaani mbona maisha yamekwama. Baadhi yetu tunaamini tumefanikiwa mbele
ya macho ya watu kwa kumiliki vitu vya thamani ila ukweli ni kwamba mafanikio
ni zaidi ya hayo.
Kwa
maneno yasiyokuwa rasmi mafanikio ni kuwa vile unavyopenda kuwa na kunufaika na
kunufaisha wengine kwa vile unavyovipenda. Ukweli ni kwamba wengi tunatumia
nguvu nyingi kutafuta vitu ili kuridhia macho ya watu au tu kusongesha maisha
mbele, ila pengine hata hatufurahii kile tunachokifanya isipokuwa ni mfumo na
msukumo tu wa maisha ndio unatulazimisha kuwepo hapo na hatuna namna.
Hakuna
jambo bora sana katika maisha kama kufanya jambo ambalo unalifurahia na
linakuletea kipato. Jambo amabalo unaingoja asubuhi ili uamke na
kulifanya,jambo ambalo hautamani jua lizame kabla haujamaliza. Na hili ndilo
kusudio la maisha linautosheleza moyo ,linatosheleza wengine na linaleta
kipato. Kipato hufuata tena kikubwa na kwa kasi kubwa hasa unapofanya jambo
sahihi kwa wkati sahihi ambalo ni kusudio la kuwepo kwako.
Upo duniani kwa lengo
maalum, ligundue leo!
Kila
mmoja katika hii dunia ana lengo na kazi maalumu ya kufanya ambayo hakuna mtu
mwingine yoyote aliletwa kuifanya. Kama ambavyo alama za vidole (finger prints) zilivyo tofauti; basi na
lengo la kuwepo kwako duniani ni tofauti na la mwingine, japokua kwa mbali sana
linaweza onekana linafanana na mwingine.
Kujua
lengo au kusudio la maisha yako inakupasa; kujua ni kitu gani unakifanya vizuri
zaidi, watu wanapenda nini toka kwako, kitu gani una shauku nacho kila
inapoitwa leo. Geuka nyuma na tafakari na kukumbuka.
1. Ni
kitu gani huwa unashauku ya kukifanya na huwa ni kirahisi sana kukifanya hata
kama wengine wanakiona kigumu na wanashindwa pengine?
2. Jambo
gani unachukia sana unapoona mtu mwingine anakifanya kwa makosa wakati wewe
unaweza kukifanya vizuri sana?
3. Kitu
ambacho unapenda kukifanya hata kama hautalipwa unaendelea kukipenda?
Kuna zawadi kubwa sana ndani yako
itafute, ifanye iwepo ikufanyie kazi na uifurahie,itabadili maisha yako na ya
wengine na hii ndio njia ya kutafuta na kupata kusudio la maisha yako.
Katika
kufikia kusudio la maisha yako fuata hatua zifuatazo itakusaidia.
Jione
wewe uliefanikiwa yaone mafanikio yako. Hii itakusaidia kuongeza jitihada
kufikia mafanikio.Picha kubwa hii unaiona katika jambo ambalo unalipenda na
kuliweza. Mfano unajiona upo uwanja mkubwa unacheza mpira na timu kubwa Afrika
au duniani. Endapo tu unapenda na unajua kucheza mpira. Hii itatoa hamasa ya
kufanya mazoezi na kuweka juhudi katika kufikia lengo na kusudio la maisha yako
ya mafanikio. Cameron Johnson mzungumzaji na mshauri wa makampuni Zaidi ya 500
makubwa duniani moja ya nukuu zake aliwahi kusema “Usiogope kukataliwa ,usitafute
sababu ya kushindwa ,anza kidogo, tia mkazo kufanya mambo mazuri na kila kitu
kitafuata .Kila kitu kina kujifunza na mwishowe mafanikio huja kama mfumo wa
maisha”.Kikubwa ni kuanza na kufanya katika usahihi utashangaa jinsi
mafuriko ya mafanikio yanavyokupata.
Hatua ya pili: Weka
nguvu na mkazo katika yale unayotaka kufanya.
Chukua
hatua walau ndogo ,thubutu kufanya walau kidogo,weka mikakati na usiogope
kujikwaa ama kuanguka. Ni sehemu ya mafanikio kwa maana utakua umejifunza.Kwa
kuwa sasa unajua nini unaweza na nini unataka na wewe ni nani.
Kwa
kuwa na uhakika na hilo ,sasa unaweza kuchukua hatua maana mafanikio yako yapo
ndani yako.Kumbuka ni hatua ya kwanza ndio jambo kubwa Zaidi.Haitatokea miujiza
ya kufanikiwa kufikia kusudio la maisha kabla haujachukua hatua yoyote ,kwa
kushindwa kufanya hivyo utabaki hapo ulipo na labda utapiga hatua nyuma.
Hatua ya tatu: Songa
mbele.
Haijalishi
ni ngumu kiasi gani, hakuna jambo zuri lilikuja kwa urahisi. Usiruhusu mawazo
ya watu wengine yakubomoe hali ya kua unaamini kile unachokifanya ni sahihi.
Kumbuka kila mtu ana historia ya maisha yake. Fikiria nje ya sanduku na amini
wewe ni Zaidi ya ulivyo.Tumia akili yako yote na uwezo wako wote kulisimamisha
hilo unaloliamini maana hilo ndio wewe.Katika jamii kila mmoja huwa na maoni
yake juu ya kila tukio ambalo linatokea. Wapo ambao kwa mawazo yao huamini
haitakaa iwezekane jambo Fulani kutokea. Ila kwa kuwa wewe unaweza na unaamini
unaweza basi ni kweli unaweza.
Katika
jambo ambalo upo mahala sahihi na unatia jitihada basi hata Mungu husimama
nyumba yako na kukuandalia majeshi ya kukuvusha salama . Hotuba ya Mwalimu
Julius Nyerere aliyoitoa tarehe 2 Novemba, 1978 alipokuwa akitangaza vita vya
kupambana na uvamizi wa majeshi ya Idd Amini katika ukumbi wa Diamond Jubilee,
alisema kauli ya “…………Uwezo wakumpiga tunao. Sababu ya kumpiga
tunayo. Na nia ya kupiga tunayo……..”
kwa kuamini hivi ndivyo ilivyokuwa
na ushindi mkubwa ulipatikana. Unapokuwa na nia sababu , na uwezo kwa nini
ushindwe?
Hatua ya nne: Weka
vipaumbele katika mambo ya msingi.
kila
jambo unatakiwa ufanye ,si kila biashara nzuri iliyomletea mtu Fulani mafanikio
basi na wewe utapata nalo mafanikio. Tengeneza mtandao wako wa watu na ushirika
na watu ambao watakua na wewe katika mchakato. Moja ya mambo niliyowahi
kujifunza ni kwamba unapotaka kufika mahala Fulani ikiwa ndio sababu ya uwepo
wako basi kuna watu waliumbwa na wao lengo la kuwepo kwao ni kuhakikisha lengo
lako linatimia, na kama haujachukua hatua basi kuna idadi kubwa ya watu wanaangukwa
kwa wewe tu kutokufanya hivyo.
Wao
wanatakiwa kufikia kusudia la maisha yao ila wewe ni sehemu ya kusudio lao kama
wao walivyo sehemu ya kusudio lako. Unaweza kuwa na wazo pan asana na pengine
wewe pekee usitoshe na unahitaji watu wa taaluma mbali mbali basi hao ndio wa
kuwatumia na muweze kusafiri pamoja kila
mtu kufika kusudio la maisha yake. Mwandishi Winston Churchill aliwahi kusema ….tunajenga
majengo yetu ,na majengo yetu hutujenga.” Kusudi ya kauli hii ya bwana
Churchill ni kwamba kile ambacho tuanakifanya leo ndio picha halisi ya kesho
yako.Fanya kazi leo ,tena kwa nguvu sana na kesho utafurahia kwa dhifa kubwa.
Hatua ya Tano: Tengeneza
brand ya kusudio lako.
Kumbuka
unachofanya ni cha kwako basi kifanye kwa namna yako na si kwa namna ya
mwingine kuwa wa kipekee hata kama mwingine anafanya si lazima ufanye kama yeye
kwa sababu yeye sio wewe. Be “you”nique.
Jifunze
tena na tena ili kujiimarisha kwa unalotaka kulifanya. Kuna tofauti kubwa sana
kati ya ukweli wa wewe ulivyo na nini kipo ndani ya watu
wanaokutazama.Tengeneza picha yako.
Hatua ya Sita: Endelea kujiboresha leo ,kesho na kila
siku.
Usijifunge
hapo jaribu kukua na kufanya jambo jipya kila unapotaka au inapohitajika
kufanya hivyo. Na mara nyingi unapofanya jambo ililoumbwa kwalo basi utaendlea
kufanya licha ya ugumu wowote kaa tulivyosema awali kitu amabacho hata
usipolipwa una nraha kufanya. Na hili litatoka kuwa jambo unalolipenda tu mpaka
jambo lenye kuleta faida kubwa.Tumia teknolojia ni msaada mkubwa Kuwa mbunifu Kwa
hatua hizi kwa kuwa na ustahimilivu na jitihada itapelekea mafanikio kutokea
kwa wakati. Ama ni biashara au aina yoyote ya shughuli ya kupata kipato basi
ona kwamba hilo ni jambo lako na ndilo unalopaswa kulifanya ndilo
unalolimiliki.

Kwa
maneno ya Siddhārtha Gautama,mwanafalsafa
,mwalimu na kiongozi ya dini ya kibuddha "Kusudio lako maishani ni kupata
kusudi lako na kutoa moyo wako wote na roho yako yote kwenye kusudio hilo"
Siddhārtha Gautama
……………………….
Mwandishi
ni mkurugenzi wa Umoja Creatives Company na Mkufunzi wa Uongozi na Menejimenti.
Mawasiliano: +255 716 050 555, +255 754 686 393, abbshey09@gmail.com
…………………………..
No comments:
Post a Comment