Imeandikwa na Abdallah Wihenge
Kutokana na changamoto za ajira ambazo zinazikumba nchi nyingi hasa za ukanda wa Afrika pengine na maeneo mengi duniani ,pamekua na mihehemko hasa kwa jamii maskini juu ya kujikwamua kutoka katika wimbi la ukosefu wa ajira na kipato.
Changamoto hii imepelekea wengi katika vijana
pengine na watu wengine wakijikuta kwa kupapasa tu na bila kutumia nyingi
katika fikra zao kutafakari juu ya nini na wakati gani wafanye nini. Suala hili
limepelekea watu wengi kujikuta kila fursa au inayoitwa fursa basi na yeye
ataingia kwa kiu tu ya kupata kipato au ujira ili kujikwamua kitoka kaika wimbi
la umasikini.
Katika makala hii nitagusia maeneo kadhaa katika
utimamu wa kuchagua fursa za kibiashara na kijarisiamali. Na ikumbukwe kwamba
kila mtu ana kusudi katika maisha kwa maana sababu ya kuwepo kwake, na ndio maana
binadamu wote hawawezi kufanya kila kitu na kila jambo. Hii ina maana hatokuwepo
mtu wa kuwa mwalimu yeye, daktari, mkulima, mvuvi, mkandarasi kwa wakati mmoja..
Katika makala zilizozopita zilieleza wazi juu ya
kusudi la maisha , na ni kupita makala hizo na nyinginezo utajua nini kusudio
la maisha yako na kuanzia hapo utapata njia ya kusonga na kupiga hatua katika
maisha kwa kujua wewe ni nani na unataka kufanya au unatakiwa kufanya nini
duniani.
Katika harakati za kujikwamua kila mmoja ana
namna ya kipekee ambayo anaitumia kuelezea namna ya kujikwamua.Mathalani yapo makundi yanaamini katika biashara ya
mtandao na faida zake katika kujikwamua,wapo watu wanaamini juu ya biashara ya
kilimo na mazao na wanaijua jinsi ilivyo, biashara ya udalali ,vifaa vya umeme
na nyingine nyingi.
Hizo zote ni biashara nzuri ila ikumbukwe kwamba
si kila biashara ni ya kila mtu kuifanya,hata kama ni rahisi kiasi gani.
Zingatia mambo yafuatayo unapochagua aina ya biashara ya kufanya.
- Haijalishi ni ushawishi kiasi gani unapewa na mtu au mtu juu ya kufanya biashara husika.Fanya kile ambacho unakiamini hata kama hakuna anaekiamini.Kuna watu wana uwezo mkubwa sana wa ushawishi na kutia moyo hata kukufikisha pahala ukaona upande chanya wa jambo na kujikuta unaingia.Ushawishi hasa kwenye jambo la kibiashara ni vyema sana ila washawishi wanapaswa kujua kwamba watu wanatofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine.
- Ili uweze kufanikiwa katika
jambo lolote ama ni zuri au baya ,hatua ya mwanzo kabisa ni kuliamini kutoka
ndani ama kwa kuambiwa ama kwa kulitafakari mwenyewe.Isitoshe tu kupokea
ushawishi kutoka kwa watu na ukakubali eti kwa kuwa umeambiwa ni zuri,kumbuka kuchukua
muda wakao kulitafakari na kujiuliza maswali na majibu juu ya uhusiano wake na
kusudio lako.
Wengi wamejikuta wakiangukia
katika kila biashara na kupoteza pesa kwa changamoto ya kuparamia na ushawishi wa
hali ya juu katika biashara fulani fulani.Mfano katika miaka ya hivi
karibuni wakina dada wengi waliopo kwenye ajira rasmi na wale waliojiajiri
wamejikita katika biashara ya mikoba na vipodozi. Ni biashara nzuri ndiyo ,Ila
wengi waliojikita katika biashara hii ni kutokana na msukumo kutoka kwa
marafiki pia na mitandao.Hii inapelekea katika sehemu moja ya kazi pengine
yenye watu kumi basi watatu wanafanya biashara inayofanana jambo ambalo
linapelekea kujidumaza kibiashara na kipato pia kwani mzunguko wa wateja ni ule
ule.
- Pia mlipuko wa biashara ya mtandao ya kwamba, njoo na mtu utapata kiasi fulani kwa uwepo wake. Hii ni moja ya biashara nzuri pia na inafanyika maeneo mengi duniani.Changamoto ni kwamba waelezeaji wa biashara hii huelezea upande mmoja tu wa biashara ,upande wa kupata na wanaacha changamoto na madhira yake nyuma.Ni vema kabla ya kuingia katika bishara hii mbali na ushawishi na msukumo mkubwa kupata muda wa kutafakari na kujiridhisha na kujifunza kwa waliowahi kufanya katika meneo mengine na walifanikiwa kwa kiasi gani.
Wengi wamepoteza pesa na wengi wapo kwenye mapambano ya kurejesha kiasi cha pesa
walichowekeza bila kujua hatma yake.Wengi hujikuta wanakomaa na kuendelea
kupambana na kuupoteza muda kwa kutaka kuhakikisha kiasi cha pesa
kinarejea na anaendendea kupoteza fursa nyingine kutokana na mkwamo huu huu.
Ni hivyo hivyo
katika biashara nyingine kama kilimo, ufugaji, uwekezaji na kadhalika. Si vibaya
kushindwa kwani ni kujifunza ila kushindwa katika jambo amabalo haukuiruhusu
akili yako kutafakari ni kushindwa kiwango kibaya zaidi.
- Usichague biashara kwa kigezo cha kujipatia pesa (nyingi) tu.Ni kweli misukumo mingi ya watu juu ya kufanya biashara ni kuhakikisha wanapata pesa za kujikwamua kiuchumi tu.Biashara au shughuli unayoifanya inapaswa kukupelekea kupata kipato cha kujikwamua ,ila jambo hili likibaki kama ndio lengo kuu na la pekee la kufanya biashara husika, basi kwa asilimia 50 tegemea kutofanikiwa na kuanguka.Wengi waliingia kwenye biashara kwa kushawishiwa na uchu wa kupata pesa. Pesa ni zawadi inayokuja baada ya kufanya jambo jema na sawa, na baada ya kufikia kusudio la maisha yako.Unaonaje kupata pesa kutoka katika kitu au biashara unayoifurahia? Utajisikaje kupata pesa katika jambo ambalo unaona asubuhi inakawia kufika ili ukafanye?Unaonaje kuutumia usiku na mchana wote kufanya kitu ambacho unakipenda na kinakuletea pesa zinazoyafanya maisha yako?
Hii ndio
tafsiri ya aina ya biashara na shughuli ya kukupatia kipato unayopaswa
kuifanya.
- Jamii hasa vijana imejikuta katika wimbi la kufanya biashara kwa ajili tu ya kujionesha kwa watu kwamba nao hawajakaa bure kuna biashara ‘mishemishe ‘ wanafanya mjini.Jambo hili linapelekea kujikuta wameangukia kwenye biashara yoyote ,na hatma yake ni kuanguka na kushindwa kujikwamua kiuchumi. Hakuna anaejali ni nini unafanya hali ya kuwa hakina manufaa au hakina tija kwako au kwa jamii yako. Unahitaji kukaa chini kutafakari na kuchanganua chochote ambacho unakitizamia kukifanya ili kikuletee kipato.Ni ngumu kufanikiwa katika jambo usilolijua ama kwa bahati nasibu ambayo nayo haitakuja mpaka uwe katika mazingira ya kuipata bahati.
- Kuiga toka kwa watu, Hili pia ni janga kubwa hasa kwa jamii ya wazawa wa ulimwengu watatu. Mathalani elimu tuliyoipata na jamii tulizotokea hazikutuandaa kuweza kufanya maamuzi ya biashara gani au shughuli gani ya kipato yatupasa kuifanya. Hii inapelekea kuiga kwa ‘sisisi’ kutoka kwa watu wanaofanya aina fulani ya biashara. Mfano bwana fulani alifanikiwa kwa biashara ya duka la rejareja mtaani kwake , na kijana mwingine wa mtaa mwingine akaona mafanikio hayo na agharabu ana mtaji wa kumuwezesha kufanya aina hiyo ya biashara husika basi bila ya kufanya tafakari kwa yakini ,anachokitizama mbele yake ni mafanikio na sasa anakwenda kujikita katika biashara hiyo , na pengine katika mazingira yasiyo sahihi ama mbinu zisizo sahihi na anaanguka. Ni vema kujifunza na kujihakikishia juu ya kile unachotaraji kukifanya.
- Maamuzi ya biashara moja kwa wakati mmoja ni bora zaidi kwa kuanzia.Changamoto nyingine inayowagharimu watu wengi ni kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja.Utaona ajabu unakutana na mtu ndani ya mwezi mmoja ameshafanya takribani biashara tatu na mbili zilikwishashindwa na moja ndio anayoifanya na inaelekea kushindwa.Pengine ni tamaa au shauku ya kufanikiwa ndio msukumo wa hadha hii.Moja ya jambo kubwa ni kuweza kuwa na uwezo wa kusimamia akili binafsi.Kufanya biashara nyingi kwa wakati mmoja inapelekea kukosa kumakinika katika wazo moja la biashara na pengine maisha kwa ujumla. Kutumia muda mwingi kupigania wazo moja ni bora zaidi ya kuutumia muda huo kufanya mambo mengi yasiyo na tija.
- Kujijengea uwezo wa kuyachanganua na kuyafanyia kazi maudhui ya wahamasishaji “motivational speakers”.
Hawa ni watu muhimu sana na wamekuwa ni msaada mkubwa sana katika
kutia chachu ya kuwaamsha watu katika suala zima la maendeleo na kujikwamua,
pia ni wazi kwamba wao hufanya shughuli zao kwa makundi ya ujumla hali ya kuwa
uwezo wa uchanganuzi na uelewa wa watu unatofautiana.Watu wengi husikiliza
maudhui yanayokuja mbele zao hasa juu ya masuala ya biashara na kwa sababu
wamehamasika basi hunyanyuka na hamasa na kufanya maamuzi ya kufanya chochote
katika biashara, na pale hamasa inaposhuka anajikuta kumbe alichagua biashara kwa
mihehemko ya hamasa na alisahau kuushirikisha ubongo wake katika maamuzi. Ni
vema kuweka nukta na kutafakari kwa kina kila ambacho unahamasishwa nacho na
baadae kuamua maamuzi ambayo hautajutia. kabla ya kuamua maneno mazuri ya wahamasishaji:
1.
Sikiliza
na kwa makini maudhui yao
2.
Tenga
muda wa kutafakari na kuamua
3.
Amua
kwa moyo mmoja maamuzi yaliyo sahihi.
Pamekua na aina fulani ya watu
ambao wao hufanya biashara inayo ‘trend’. Hili ni jambo zuri na ni fursa
pia.Kufanya biashara ambayo inahitajika kwa wakati huo ni njia nzuri ya
kukusanya kipato kwa ajili ya biashara ambayo utaishi nayo.Changamoto ya
biashara za namna hii ni kukutoa katika mstari wa biashara yako ya kudumu.Hii
inapoteza malengo yako ya muda mrefu na kujikuta unakwenda kutumia nguvu,akili
na mali nyingi kupambana na jambo la msimu na kisha baada ya hapo unarudi
kuanza moja katika biashara ya kudumu.Mara nyingi biashara hizi hufanywa na
kila mtu na faida yake huwa ni ndogo ukilinganisha na rasilimali
zitakazowekezwa.
Muda ni mali na ni vyema
kuutumia kuboresha jambo kuu la msingi kuliko kushughulika na mambo madogo madogo
yanayotumia rasilimali muda zaidi.
Katika Makala zitakazofuata
tutatizamia namna gani ya kuanza kidogo katika biashara kwa kutumia mtaji
kidogo na maarifa mengi,